MKURUGENZI MKUU BODI YA UTALII ASIMAMISHWA KAZI


Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Damas Ndumbaro amemsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Devota Mdachi kupisha uchunguzi wa madai ya matumizi mabaya ya fedha na rasilimali katika ofisi yake.

Waziri Dkt.Ndumbaro ametoa uamuzi huo leo mkoani Dar es salaam ambapo amesema uchunguzi huo hauhusiani na ripoti ya hivi karibuni iliyotolewa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Amesema kwa sasa nafasi ya Mdachi itakaimiwa na Betrita James ambaye ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi kutoka Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA).


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments