MWANAFUNZI WA DARASA LA SABA AUAWA AKITUHUMIWA KUIBA SHILINGI ELFU 15

Mwanafunzi wa darasa la saba katika shule ya Msingi Kalangalala iliyopo mjini Geita ameuawa kwa kupigwa mateke na ngumi akituhumiwa kuiba Sh 15,000 kwenye duka lililopo jirani na nyumba yao.

Kamanda wa polisi mkoa wa Geita Henry Mwaibambe amesema tukio hilo limetokea Aprili 7,2021 wakati mtoto huyo akipatiwa matibabu katika hospitali ya mkoa wa Geita.

Kamanda amesema mtoto huyo alishambuliwa na mwenye duka Hamad Juma aliyetoroka baada ya tukio hilo na jeshi la polisi linamsaka.

“Mtoto huyu inadaiwa alikuwa anaiba dukani na mtuhumiwa alimkamata na kumuadhibu sehemu mbalimbali za mwili na kusababisha kifo chake”amesema Mwaibambe.

Chanzo - Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments