Shirika la Reli Tanzania (TRC) limethibitisha kutokea kwa ajali ya treni leo alfajiri eneo la Vingunguti, Dar es Salaam ambapo gari la mizigo limeigonga treni kwenye kivuko cha reli na barabara.
TRC imeeleza kuwa katika ajali hiyo hakuna taarifa za kifo na kuwa majeruhi ni watatu, wote wafanyakazi wa TRC, na tayari wamepelekwa hospitali ya Reli Tanzania kwa matibabu.
Treni hiyo ya abiria (Deluxe) ilikuwa ikitokea mikoa ya Kigoma, Tabora, Dodoma na Morogoro na wakati wa ajali ilikuwa na abiria wapatao 828.
Shirika hilo mbali na kutoa pole kwa waliofikwa na ajali hiyo, limeendelea kusisitiza umma kuzingatia sheria za barabarani kwani dereva wa gari lililogonga treni alitakiwa kupunguza mwendo na kusimama umbali wa mita 100 alipokaribia kivuko hicho.
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin