MBUNGE wa Viti Maalumu anaewakilisha
Kundi la Asasi za Kiraia (NGOs) CCM Neema Lugangira amesema kwamba Sekta
ya Azaki bado inahitaji kujengewa uwezo haswa NGOs ndogo ili ziweze
kutekeleza majukumu yao kwa tija kubwa .
Hayo
aliyasema wakati alipokutana na Mashirika yasiyokuwa ya
Kiserikali(NGOS) kwa upande wa Tanzania bara kwenye Kikao Kazi cha
Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto na Mashirika hayo.
Kikao
hicho ambacho amekutana na Sekta ya Azaki (NGOs) kwa mara ya kwanza,
Mbunge Neema alisema ushirikiano kati ya Bunge, NGOs na Serikali ni
muhimu kwakuwa wote ni wadau wa maendeleo na kazi yao ni kuhudumia
wananchi.
Mbunge
Neema Lugangira alipendekeza mambo mawili; kwanza NGOs kubwa za Kitaifa
ziwe na utayari wa kufanya kazi na NGOs ndogo na pili NGOs za Kimataifa
na Wadau wa Maendeleo waelekezwe juu ya umuhimu wa kuhakikisha sehemu
ya fursa walizonazo zinakwenda kwa NGOs ndogo.
Alisema
kwamba hiyo yatasaidia kuwajengea uwezo NGOs ndogo na hatimae kujenga
mazingira wezeshi ya NGOs ndogo ili nazo zikue na kutimiza malengo yake
vizuri.
Mbunge
Lugangira huyo alisema ili NGOs ziweze kuthaminika na kutambulika kwa
kazi kubwa inayofanyika katika kuleta maendeleo kwa jamii ni lazima NGOs
zifanye kazi kwa uwazi na uwajibikaji.
“
Kwani kwa kufanya hivi pamoja na mambo mengine, itaiongezea nguvu hoja
zinazowasilishwa na Sekta hii muhimu ya NGOs kwenda Serikalini na
Bungeni” Alisema Mbunge huyo.
Hata
hivyo Mbunge Neema alitoa ushauri kwa Baraza la Taifa la Mashirika
Yasiyo Ya Kiserikali "NACONGO" ianze kutekeleza muundo wake wa kuwa na
uwakilishi wa NGOs ngazi zote kuanzia Wilaya, Mkoa hadi Taifa kupitia
Mabaraza ya Wilaya, Mikoa hadi Taifa.
“
Hii itasaidia kuratibu mipango ya Serikali na NGOs kwenda sambamba na
pia hili litanisaidia sana mimi kama Mbunge wa Viti Maalumu
ninaewakilisha kundi la NGOs Bungeni maana ninahitaji kukutana na NGOs
Wilayani, Mikoani na Taifani kupitia mfumo rasmi kama huu wa NACONGO
hivyo ni muhimu sana Mabaraza haya ngazi zote yawepo na yafanye kazi”
Alisema Mbunge huyo.
Mbunge
huyo aliwahakikishia Wadau wa Sekta ya NGOs kuwa atakuwa Mwakilishi wa
Mashirika Yasiyo ya Kiserikali/Asasi za Kiraia (NGOs) Bungeni ikiwemo
kuwa tayari kushirikiana nao kuimarisha Sekta hiyo ya Azaki.
“Lakini
pia niliwasilisha ombi langu la kushirikiana kwa karibu na Foundation
for Civil Society kwa lengo la kufanyia kazi haya niliyowasilisha na
mengine ambayo tutayajadili pindi tutakapokutana” Alisisitiza
Katika
hatua nyengine Mbunge huyo aliwashukuru Wakurugenzi Wanawake 7 wa NGOs
kutoka Jukwaa la Wakurugenzi Wanawake wa Azaki "CSO Women Directors
Forum" ambao walikubali kutenga muda wao, kupitia na kuboresha maelezo
yangu hadi kufanya zoezi la kuomba kura mbele yao ili kuhakikisha
nitakuwa ndani ya muda.
Wakurugenzi
hao ni Anna Kulaya, Jane Magigita, Dr. Astronaut Bagile, Christina
Kamili, Geline Fuko, Utti Mwangamba na Irene Fugara.
“Kwa
hakika huu ulikuwa Mkutano muhimu sana kwangu kushiriki na namshukuru
sana Mhe Spika, Mhe Job Ndugai (Mb.) kwa kunipa ruhusa ya kutoka Bungeni
na kushiriki Mkutano huu” Alisema Mbunge huyo
Aidha
pia aliwashukuru Mhe Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee
na Watoto, Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima, Mhe Naibu Waziri, Mhe Dkt. Mollel
na Katibu Mkuu wa Maendeleo ya Jamii, Dkt. Jingu kwa ushirikiano wa
mkubwa na kwa utambuzi wa nafasi yangu kama kiungo muhimu kati ya NGOs,
Serikali, na Bunge.
"Sasa
kazi iendelee na tuachane na tofauti ya itikadi zetu za kisiasa,
tufanye kazi na mnitumie kama daraja kati yenu NGOs, Bunge na Serikali",
alihitimisha Mbunge Lugangira
Mwisho
Post a Comment