UCHAGUZI WA MAREKANI 2020: MCHUANO BADO MKALI KATI YA TRUMP NA BIDEN


Matokeo ya awali ya urais nchini Marekani kati ya Donald Trump na hasimu wake wa Democrat Joe Biden yanaonesha mchuano kuwa mkali katika majimbo kadhaa.

Donald Trump anaongoza katika jimbo la Florida kwa karibu kura zote zilizohesabiwa.

Lakini majimbo mengine ya Georgia, Pennsylvania, Wisconsin, Michigan, Arizona, Ohio, Texas, na North Carolina chochote kinatarajiwa.

Zaidi ya watu milioni 100 walikwisha piga kura zao za mapema.

Udhibiti wa Congress pia uko hatarini. Pamoja na Ikulu ya White House, Republican wanawania kupata idadi kubwa ya viti vya Seneti.

Bunge la wawakilishi linatarajiwa kuwa katika mikono ya Democratic.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments