KIJANA ABUNI KOFIA MAALUM KWA AJILI YA MBWA


Mkurugenzi wa sanaa kijana Rajeev Basu nchini Marekani ametengeneza kofia maalumu kwa ajili ya mbwa wenye usingizi. Bei ya kila kofia ni kati ya dola za kimarekani 500 hadi 550.

Alimuona mbwa wake aitwaye Remy akisinzia hadi kuanguka, hivyo akaamua kubuni kofia maridadi iliyomfanya mbwa ajisikie vizuri.

Rajeev Basu amesema kofia hizi zinaweza kuwatia mbwa joto kila mahali na kulala wakati wowote. Kila kofia ni ya kipekee na imetengenezwa kwa mikono huko New York.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments