BARAZA LA MAWAZIRI KUKOMA SHUGHULI ZAKE LEO


Msemaji Mkuu wa Serikali, Dk. Hassan Abbas

Na Richard Mwaikenda,  Dodoma

BARAZA la Mawaziri limekoma leo kuendelea na shughuli za kikazi mara atakapoapishwa Rais Mteule, Dk. John Magufuli kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.

Taarifa hiyo imetolewa na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dk. Hassan Abbas alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari jijini Dodoma jana, kuhusu kukamilika kwa maandalizi ya kuapishwa kwa Rais Mteule, Dk Magufuli.

Dk Abbas alisema kuwa kisheria ni kwamba Baraza la Mawazili la 2015-2020 mwisho wake ni mara tu Rais Mteule atakapoapishwa kushika kipindi chake cha pili cha miaka mitano. Majukumu yote yatafanywa na makatibu wakuu wa wizara hadi atakapotangaza baraza jipya.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments