TETESI ZA SOKA LEO JUMAPILI NOVEMBA 29,2020


Arsenal iko tayari kumuuza winga wa Ivory Coast Nicolas Pepe ikiwa kutapatikana mnunuaji mzuri wa mchezaji huyo, 25. (Daily Star on Sunday)

Mlinzi wa Barca raia wa Uhispania Gerard Pique, 33, anatumai kuwa klabu ya Nou Camp "itazungumza vizuri" na Messi ili asalie klabu hiyo. (ESPN)
Kipaumbele kwa Real Madrid ni kumsajili mshambuliaji wa Paris St-Germain na Ufaransa Kylian Mbappe, 21, mwaka 2021 kabla ya kujaribu kumsajili mshambuliaji wa Norway Erling Braut Haaland, 20, kutoka Borussia Dortmund mwa 2022. (AS)

Manchester City imekuwa ikimnyatia Martinez kwa zaidi ya mwaka huku Barcelona na Real Madrid pia zikionesha nia ya kumtaka mchezaji huyo, 23. (Sunday Mirror)
Chelsea "inatathmini" ikiwa itamsajili mshambuliaji wa Argentina Lionel Messi kama mchezaji huyo, 33, ataondoka timu ya mabingwa Uhispania Barcelona. (Spanish football expert Guillem Balague, via Sunday Express)

Mkuu mtendaji wa Inter Milan Giuseppe Marotta amesema kuwa kiungo wa kati wa Denmark Christian Eriksen, 28, ataondoka klabu hiyo Januari wakati dirisha la usajili litakapofunguliwa. (Sky Sports)
Philippe Coutinho ameiwakilisha Brazil mara 55

Ajenti wa kiungo wa kati mshambuliaji wa Brazil Philippe Coutinho anasema mchezaji huyo, 28, hana mpango wa kuondoka Barcelona baada ya kuhusishwa na upande wa Italia Juventus. (Mundo Deportivo - in Spanish)

Ajenti wa Domenico Berardi wa Sassuolo anasema mshambuliaji huyo wa Italia thamani yake ni euro milioni 50 na kwamba mchezaji huyo, 26, hana mpango wa kulazimisha kuondoka upande wa Serie A. (Football Italia)
Mshambuliaji wa Inter Milan Lautaro Martinez

Mshambuliaji wa Argentina Lautaro Martinez anataka kuondoka Inter Milan na amemuweka ajenti wake Jorge Mendes kusimamia utafutaji wa klabu mpya atakayo hamia. (Marca)

Watu sita wameonesha nia ya uwezekano wa kununua klabu ya West Bromwich Albion lakini mmiliki wa klabu hiyo Guochuan Lai huenda akawa na wakati mgumu wa kufikia lengo lake la kuiuza kwa pauni milioni 150 kwa klabu hiyo ya Ligi ya Premier. (Mail on Sunday)
Mkurugenzi wa michezo wa Borussia Dortmund Michael Zorc anasema anatazamia kumuona mshambuliaji wa Norway Erling Braut Haaland katika klabu hiyo "kwa muda mrefu". Nyota huyo aliye na miaka 20- ana mkataba na klabu hiyo ya Bundesliga hadi mwaka 2024, lakini anaweza kuondoka kwa euro milioni 75 (£67m) mwaka 2022 kwasababu ana kifungu kinachomruhusu kufanya hivyo katika mkataba wake wa sasa. (Bild Sport - in German)

Winga Muingereza Angel Gomes, 20, anasema aliondoka Manchester United 'kutafuta mwanzo mpya' baada ya kukataa ofa yao na kujiunga na Lille. (Independent)

Matej Vydra (Kulia) amekuwa na Burnley tangu mwaka 2018

Mshambuliaji wa Burnley na Jamhuri ya Czech Matej Vydra, 28, anataka kuondoka Turf Moor ili kupata nafasi ya kucheza soka ya kikosi cha kwanza. (Accrington Observer)

Mkufunzi wa zamani wa Manchester United Sir Alex Ferguson ameahidi kuongeza msaada wake wa chakula kwa shirika la watoto na kutoa wito kwa wachezaji zaidi wa soka kumsaidia mshambuliaji wa England na United Marcus Rashford, 23, katika kampeni yake ya kuwakinga watoto dhidi ya njaa. (Times - subscription required)

Mshambuliaji wa Manchester United Marcus Rashford anasema kusaidia watoto "ni muhimu sana" wakati wa Janga la corona

Beki wa kushoto na nyuma wa Argentina Nicolas Tagliafico ambaye amehusishwa na Chelsea na Manchester City, amekubali kurefusha mkataba wake na Ajax ambayo unatarajiwa kumfanya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 kusalia katika klabu hiyo hadi angalau mwisho wa msimu . (De Telegraaf - in Dutch)

Kipa wa Fulham Marcus Bettinelli, 28, ananyatiwa na klabu kadhaa za Ligi ya Primia. Kipa huyo ambaye kwa sasa yuko Middlesbrough kwa mkopo alijumuishwa katika kikosi cha kitaifa cha England na Gareth Southgate mwaka 2018. (Mail)

CHANZO- BBC SWAHILI

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments