Pia, Dk. Msonde amewataka wasimamizi wa mitihani hiyo kufanya kazi kwa uadilifu na kulinda haki ya watahiniwa.
“Baraza linatoa wito kwa wasimamizi wote walioteuliwa kwa ajili ya kufanya kazi hiyo, wafanye kwa uadilifu wa hali ya juu na wahakikishe wanalinda haki za watahiniwa wenye mahitaji maalumu” amesema Dk. Msonde.
Aidha, Dk. Msonde amewataka wamiliki wa shule kutambua kuwa shule zao ni vituo maalum vya mitihani, hivyo hawatakiwi kwa namna yoyote ile kuingilia majukumu ya wasimamizi wa mitihani.
Post a Comment