Chama cha ACT-Wazalendo kimeeleza kuwa kiongozi wa chama hicho, Zitto Zuberi Kabwe amepata ajali ya gari akiwa njiani akitokea Kata ya Kalya kuelekea Lukoma kwenye kampeni katika Jimbo la Kigoma Kusini
Taarifa iliyotolewa kwenye vyombo vya habari iliyotolewa na Afisa Habari ACT-Wazalendo, Arodia Peter, ilieleza kuwa ajali hiyo ilitokea jana ambapo Zitto alikuwa na watu watano kwenye gari yake.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo Zitto na watu hao ote wako salama ingawa walipata majeraha na wanahisi maumivu makali.
Taarifa hiyo ilieleza kwamba baada ya ajali hiyo walipata huduma ya kwanza kwenye eneo la ajali baadaye walipelekwa Kituo cha Afya cha Kalya kilichopo Wilaya ya Uvinza mkoani Kigoma.
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin