TIGO YAUNGANA NA ITEL KUZINDUA SIMU JANJA MPYA YA ITEL T20



Tigo tunahakikisha tunawapatia wateja wetu wote bidhaa zenye ubora wa hali ya juu kulingana na mahitaji ya wateja wetu na ndio mana leo hii tumezindua simu hii mpya #ItelT20 yenye ubora wa hali ya juu" Mkumbo Myonga-Meneja Huduma za Internet-Tigo

Tumeungana na Tigo kwa ajili ya kuwawezesha wateja wetu waweze kufurahia maisha ya kidigitali kupitia mtandao wa Tigo" Wolle Fernando-Afisa Uhusiano @itelmobiletanzania


Dar es Salaam, 2October 2020Kampuni inayoongoza nchini Tanzania kwa kutoa huduma za mawasiliano ya kidigitali, Tigo, leo imeingia makubaliano ya ushirikiano na kampuni ya utengenezaji simu za mkononi za ITEL, Transsion Holdings, na leo makampuni haya mawili yamezindua simu janja mpya za ITEL T20 ambazo zitaanza kuuzwa nchini Tanzania.

 

Mkumbo Myonga, Mkuu wa Kitengo cha Vifaa vya Mawasiliano kutoka Tigo Tanzania, amesema, “Ushirikiano wetu na Transsion Holdings tunaubeba kwa fahari kubwa kwa sababu unaenda sambamba na dira yetu ya kuhakikisha tunatoa huduma bora za kisasa kwa wateja wetu wote. Uzinduzi huu wa leo, ni wa simu nyigine ya kisasa kabisa na ya gharama nafuu ni udhibitisho kwamba kama kampuni tumejidhatiti kuhakiksha kila mteja wetu anafurahia matunda ya vifaa hivi vipya vya kisasa ambavyo vimeunganishwa na huduma bora za kidigitali zinazotolewa na Tigo”.

 

“Tuko hapa leo kuendelea kutimiza ahadi zetu kwa watanzania za kuhakikisha kila raia anafurahia kutumia simu janja za kisasa huku akiwa ameunganishwa na mtandao wa 4G ulionenea kote nchini. Simu hizi mpya zinapatikana sasa katika maduka yetu yote nchi nzima. Pia ikumbukwe kuwa simu hii ya ITEL T20 inakuja ikiwa na ofa ya GB 30 za intaneti ambazo zitatumika kwa mwaka mzima. ITEL T20 ni simu mpya yenye huduma za kisasa za simu janja zenye uwezo wa 4G na itakuwa inapatikana kwa kiasi cha shilingi 84,900/- tu”, Myonga ameeleza.




Afisa Uhusiano Kutoka ITEL,Fernando Wolle, amefurahishwa na ubia huo na Tigo Tanzania katika uzinduzi wa simu janja ya ITEL T20. “Tumeingia ubia huu na Tigo ili kuongeza thamani ya simu yetu. ITEL T20 ni zaidi ya simu janja nyingine kwa sababu imewekwa huduma nyingi za kidigitali. ITEL T20 ni simu janja yenye uwezo wa 4G ikiwa na ukubwa wa screen wa nchi tano na uwezo wa 1GB+16GB huku ikiwa inafanya kazi kwa kutumia mfumo mpya wa Android P Go edition OS. Jina T20 linawakilisha, T= Tigon a 20 inawakilisha mwaka 202”, amesema Wolle.


ANGALIA TUKIO ZIMA HAPA

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments