TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAADHIMISHO YA SIKU YA CHAKULA DUNIANI


Dodoma, 01 Oktoba, 2020
Wizara ya Kilimo inapenda kuwataarifu wananchi na wadau wote wa sekta ya kilimo nchini kuwa Maadhimisho ya Siku ya Chakula Duniani yatafanyika kitaifa mkoani Njombe kuanzia tarehe 10 Oktoba 2020 na kilele chake itakuwa tarehe 16 Oktoba 2020.

Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa leo (01.10.2020) na Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Omary Mgumba jijini Dodoma imesema maandalizi ya maadhimisho hayo yamekamilika na kuwa wizara, taasisi, wakala, mashirika ya kimataifa na kitaifa zinakaribishwa kujitokeza kushiriki kwenye maadhimisho ya mwaka huu.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya Siku ya Chakula Duniani  mwaka huu inasema “Kesho Njema Inajengwa na Lishe Bora Endelevu” .

Imetolewa na;
Revocatus Kassimba
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527