MKE WA WAZIRI MKUU MSTAAFU DK SALIM AHMED SALIM KUZIKWA KESHO

 Mke wa Waziri Mkuu mstaafu, Dk Salim Ahmed Salim, Amne Salim anatarajiwa kuzikwa kesho katika makaburi ya Kisutu ,jijini Dar es Salaam.


Amne alifariki dunia usiku wa kuamkia jana baada ya kulazwa katika hospitali ya Aga Khan kwa muda.

Amne alijaliwa kupata watoto watatu na Dk Salim aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa iliyokuwa Jumuiya ya Umoja wa Afrika (OAU). Watoto hao ni Maryam, Ali na Ahmed.

Mbali na kuwa kiongozi wa OAU, Dk Salim aliyekuwa mwanasiasa tangu miaka ya 1960 pia amewahi kuwa Waziri Mkuu, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa na Balozi katika nchi mbalimbali.





Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments