MGOMBEA URAIS KUPITIA CUF, PROFESA IBRAHIM LIPUMBA AAHIDI KUPAMBANA NA TATIZO LA AJIRA NCHINI


Mgombea urais kupitia CUF, Profesa Ibrahim Lipumba amesema akichaguliwa kuwa kiongozi mkuu wa nchi  atahakikisha anamaliza changamoto ya ajira nchini Tanzania.


Ameeleza hayo Jumanne Oktoba 20, 2020 katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya mji mdogo wa Mahuta Wilaya ya Nanyumbu mkoani Mtwara.


Amesema miongoni mwa ajira atakazotoa ni kuziba nafasi za watumishi wa serikali walioondolewa kwa madai ya kuwa na vyeti feki pamoja na za watumishi waliostaafu na kufariki dunia.

Amedai nafasi hizo hazijajazwa  jambo ambalo linasababisha uhaba wa watumishi katika sekta ya afya na elimu.




Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments