ATUPWA JELA KWA KUFANYA MAPENZI NA KUKU HADI KUFA


Upande wa kushoto ni Rehan Baig, jamaa aliyefanya mapenzi na kuku

Mwanaume mmoja aliyefahamika kwa jina la Rehan Baig (37) Raia wa Uingereza amehukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela kwa kosa la kufanya mapenzi na kuku hadi kufa kwenye sehemu ya chini ya nyumba yao.

Tukio hilo lilitolewa ushahidi na mfanyakazi wa ndani pamoja na kamera ambazo zilinasa picha na video za jamaa huyo akifanya kitendo cha udhalilishaji kwa kuku huyo aliyekuwa na rangi ya kahawia na nyeupe.

Mahakama ya 'Bradford Crown Court' ambayo imetoa hukumu hiyo kupitia Jaji wake amesema kuwa kitendo cha tabia hiyo ni cha upotoshaji na udhalilishaji kwani mnamo siku ya Julai 9,2020 alikutwa na picha za unyanyasaji wa kingono kwa watoto.

Licha ya kuhukumiwa miaka mitatu gerezani pia amepigwa marufuku ya kutojihusisha na masuala ya wanyama na ndege kisha jina lake limeingizwa katika orodha ya watu wahalifu wa kingono wa maisha.

Source Op India.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments