TUME YA UCHAGUZI YA ZANZIBAR (ZEC) YAMTEUA MAALIM SEIF KUGOMBEA URAIS


Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), imemteua Maalim Seif Sharif Hamad kuwa mgombea urais wa Zanzibar kupitia ACT-Wazalendo katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika 27 na 28 Oktoba 2020.


Maalim Seif alikuwa miongoni mwa wagombea 17 waliokuwa wamechukua fomu kuwania urais wa Zanzibar lakini jana Alhamisi tarehe 10 Septemba 2020 ilifanya uteuzi wa wagommbea 16 na Maalim Seif akiwekewa mapingamizi.

Mapingamizi hayo yaliwekwa na vyama vya DP na Demokrasia Makini wakidai fomu za Maalim Seif aliyewahi kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar zina kasoro



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527