BABA AKAMATWA KWA KUBAKA MTOTO WAKE WA KUMZAA


Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba

Na Salvatory Ntandu - Shinyanga

Jeshi la Polisi mkoa wa Shinyanga linamshikilia mkazi wa Mtaa wa Kambarage Manspaa ya Shinyanga Petro Maro (43) kwa tuhuma ya Kumbaka mtoto wake wa kumzaa mwenye umri wa miaka 13 Mwanafunzi wa Darasa la Saba.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari Leo Septemba 29,2020 na Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba amesema kuwa Petro alitekeleza tukio hilo Septemba 27 majira ya usiku nyumbani kwake.

Alisema kuwa Mama Msamaria mwema anayeishi jirani na Petro aligundua  binti huyo kubakwa na baba yake Mzazi na kisha kutoa taarifa kwa jeshi la polisi ambao walifika na kisha kumkamata.

"Binti huyu alibakwa na baba yake usiku akiwa amelala na chanzo cha tukio hilo ni tamaa za kingono baada ya kutengana na Mke wake hali iyosababisha kuendelea kuishi na mwanae wa kike nyumba mmoja," alisema Magiligimba.

Kamanda Magiligimba alitoa wito wananchi mkoani humo kuendelea kutoa taarifa kwa jeshi la polisi ili kukomesha matukio na vitendo vya ukatili dhidi ya watoto mkoani humo.

Aliongeza kuwa hatua Kali za kisheria zitachukuliwa kwa mtuhumiwa huyo na upelelezi ukikamilika atafikishwa Mahakamani kujibu tuhuma inayomkabili.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527