TARI YATOA MAFUNZO YA AGRONOMIA YA KOROSHO KWA MAAFISA UGANI NA WAKULIMA KONGWA


Mtafiti  kutoka Tari- Naliendele Programu ya Zao la Korosho, Kasiga Ngiha, akitoa mafunzo ya jinsi ya kuandaa shamba, kulipima na upandaji wa zao la korosho kwa Maafisa Ugani na Wakulima wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa katika shamba la Shule ya Sekondari ya Mnyakongo.
Mtafiti  kutoka Tari- Naliendele Programu ya Zao la Korosho, Kasiga Ngiha, akitoa mafunzo ya jinsi ya upimaji wa shamba kabla ya kupanda korosho.
Afisa Kilimo kutoka Kata ya Songambele, Asha Malekela wa Wilaya ya Kongwa akipima shamba kwa kamba katika mafunzo hayo kwa vitendo. 

Maafisa Ugani na Wakulima wakijifunza kwa vitendo namna ya upimaji wa shamba la korosho kabla ya kupanda.
Mkulima Gasper Rupia kutoka Kijiji cha Ibwaga,  akijifunza namna ya kupima shamba wakati wa mafunzo kwa vitendo. Kulia ni Mkulima Raheli Esau kutoka kijiji hicho.

Afisa Kilimo, Said Kajagale  kutoka Kata ya Ngomai akijifunza kunyoosha mstari kwa kuelekeza kwa mkono katika mafunzo hayo ya vitendo. 
Afisa Kilimo kutoka Kata ya Mkoka, Marcelin Chingilile (kushoto) na wenzake wakiwa kwenye mafunzo hayo
Afisa Kilimo kutoka Wilaya ya Kongwa, Elias Chilemue (kushoto) na wenzake, wakijifunza kutoka TARI namna ya kuweka alama wakati wa mafunzo kwa vitendo ya upimaji wa shamba la korosho.
Afisa Kilimo kutoka Wilaya ya Kongwa, Dominica Swai (kushoto) akijifunza namna ya kuweka mambo wakati wa mafunzo kwa vitendo ya upimaji wa shamba la korosho.
Mratibu wa Kitaifa wa Zao la Korosho kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo TARI Naliendele Mtwara, Dkt.Geradina Mzena (kulia), akielekeza namna ya kunyosha mstari kwa kamba katika mafunzo hayo. 

Mkulima  Richard Sanyaji kutoka Kata ya Songambele ,  akishiriki mafunzo kwa vitendo kwa kuchimba mashimo katika shamba hilo la mfano la korosho la Shule ya Sekondari Mnyakongo.

Mkulima Gasper Rupia kutoka Kijiji cha Ibwaga,  akijifunza namna ya kuchanganya udongo na samadi kabla ya kupanda korosho.
Afisa Kilimo kutoka Kata ya Chitego, Michael Edward,  akishiriki mafunzo kwa vitendo kwa kuchimba mashimo katika shamba la mfano la korosho la Shule ya Sekondari Mnyakongo.

Mtafiti wa Kilimo kutoka  Tari Naliendele, Selemani Libaburu,  akitoa mafunzo ya jinsi ya kupanda korosho katika  shamba la mfano la korosho la Shule ya Sekondari Mnyakongo.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527