ASKOFU SANGU AOMBA MSAADA KUKARABATI KANISA KATOLIKI NGOKOLO NA MITAMBO YA REDIO FARAJA ILIYOATHIRIWA NA MVUA YENYE UPEPO


Kushoto ni Askofu wa Jimbo Katoliki la Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu,kulia ni muonekano wa sehemu ya kanisa iliyoathirika kwa kuangukiwa na mnara wa Redio Faraja

Na Simeo Makoba - Shinyanga
Askofu wa Jimbo Katoliki la Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu amewaomba wadau,waamini na watu wote wenye mapenzi mema kuguswa na kutoa michango mbalimbali ili kusaidia ukarabati wa miundombinu ya kanisa kuu la jimbo na Redio Faraja ambayo imeathiriwa na mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali.

Askofu Sangu ametoa ombi hilo katika kikao cha dharura ambacho kiliwahusisha Mapadre wa Parokia zote zilizopo katika manispaa ya Shinyanga,Viongozi wa Halmashauri ya walei kutoka kanisa kuu la Ngokolo pamoja na uongozi wa Redio Faraja Fm Stereo.

Askofu Sangu amebainisha kuwa,mvua kubwa iliyonyesha mjini Shinyanga jioni ya jana tarehe 28.09.2020 ambayo iliambatana na upepo mkali ilisababisha mnara unaotumika kurushia matangazo ya Redio Faraja Fm Stereo kuangukia kanisa na kusababisha uharibifu mkubwa wa sehemu ya kanisa na miundombinu ya Redio inayotumika kurushia matangazo.

Shinyanga limeguswa ikizingatiwa kuwa,kanisa kuu la Mama mwenye Huruma la Ngokolo ndiyo lililobeba sura ya jimbo halikadhalika Redio Faraja ndiyo chombo kikuu cha mawasialiano na uinjilishaji katika jimbo ambayo nayo miundombinu yake imeathiriwa.

Askofu Sangu amewaomba wadau wa Redio na Kanisa,Waamini na watu wote wenye mapenzi mema kuguswa na kutoa michango mbalimbali ili hatua za kufanya ukarabati wa kanisa na mitambo ya Redio iliyoathiriwa ziweze kuanza mara moja.

Ameelekeza michango yote iwekwe kwenye Akaunti maalum ya jimbo la Shinyanga Benki ya CRDB yenye namba 01J1058390001 (DIOCESE OF SHINYANGA) na kwa njia ya M-PESA kwa namba 0762444746 yenye jina la Liberatus Sangu.

Wakati huo huo, Askofu Sangu ameunda kamati maalum ambayo itashughulika na mchakato wote wa tathmini pamoja na kusimamia hatua zote za ukarabati wa kanisa na miundombinu ya Redio iliyoharibiwa,ambayo itaongozwa na Paroko wa Parokia ya Ngokolo Padre Aldof Makandagu.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mkurugenzi wa Idara ya mawasiliano wa jimbo la Shinyanga Padre Anatoly Salawa amesema hivi sasa wanaendelea na mchakato wa kurejesha matangazo ya Redio katika eneo la Shinyanga kwa kufunga Antena katika sehemu ya mnara iliyobakia ili kuwawezesha wananchi wa Shinyanga kufuatilia Matangazo ya Redio wakati hatua nyingine za kufanyia matengenezo miundombinu iliyoharibiwa zikiendelea.
Mhashamu Baba Askofu Liberatus Sangu akiwa katika eneo la tukio wakati wa zoezi la kuondoa mnara juu ya paa la kanisa la Mama Mwenye Huruma Ngokolo. Picha na Samir Salum
Mhashamu Baba Askofu Liberatus Sangu akiwa katika eneo la tukio wakati wa zoezi la kuondoa mnara juu ya paa la kanisa la Mama Mwenye Huruma Ngokolo.

Mkurugenzi wa Idara ya Mawasiliano Jimbo la Shinyanga, Padre Anatoly Salawa akionesha Mnara wa Matangazo ya Redio Faraja ulioangukia Kanisa la Mama Mwenye Huruma Ngokolo.

Muonekano wa mnara wa kurushia matangazo Redio Faraja Fm Stereo ukiwa umeangukia paa la Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo Mjini Shinyanga 
Muonekano wa mnara wa kurushia matangazo Redio Faraja Fm Stereo ukiwa umeangukia paa la Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo Mjini Shinyanga 
Muonekano wa sehemu ya ndani ya Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo Mjini Shinyanga baada ya kuangukiwa na Mnara wa Matangazo ya Radio Faraja Fm Stereo 
Muonekano wa sehemu ya ndani ya Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo Mjini Shinyanga baada ya kuangukiwa na Mnara wa Matangazo ya Radio Faraja Fm Stereo 
Muonekano wa sehemu ya ndani ya Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo Mjini Shinyanga baada ya kuangukiwa na Mnara wa Matangazo ya Radio Faraja Fm Stereo 
Muonekano wa sehemu ya ndani ya Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo Mjini Shinyanga baada ya kuangukiwa na Mnara wa Matangazo ya Radio Faraja Fm Stereo 
Muonekano wa mnara wa kurushia matangazo Redio Faraja Fm Stereo ukiwa umeangukia paa la Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo Mjini Shinyanga 
Muonekano wa mnara wa kurushia matangazo Redio Faraja Fm Stereo ukiwa umeangukia paa la Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo Mjini Shinyanga.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527