SHEMEJI AUAWA AKIAMUA UGOMVI WA MKE NA MME

Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro, linamshikilia Shinje Njilangila (30), mkazi wa Kijiji cha Mbamba, wilayani Kilosa kwa tuhuma za mauaji ya shemeji yake Dotto Ngembe (28), kwa kumchoma na kitu chenye ncha kali.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Wilbroad Mutafungwa, alisema tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia Agosti 12 baada ya Ngembe kuingilia mgogoro wa kimahusiano uliozuka baina ya mtuhumiwa na mkewe, Kulwa Ngembe, ambaye ni dada wa marehemu.

Kamanda Mtafungwa alisema mauaji hayo yalitokea nyumbani kwa marehemu ambaye alikuwa amewaita wanandoa hao kwaajili ya kusuluhisha ugomvi uliokuwa ukiendelea baina yao, ndipo mtuhumiwa alipomshambulia shemeji yake hadi kumsababishia umauti.

“Chanzo cha tukio hili mtuhumiwa alimfuata mkewe nyumbani kwa shemeji yake kwaajili ya usuluhishi, lakini ilipofika majira ya saa sita usiku ndipo alipofanya mauaji kwa kaka wa mke wake aliyekuwa akimtuhumu kuwa ndio chanzo cha mgogoro wao na baada ya kutekeleza mauaji hayo alikimbia mafichoni,” alisema Mtafungwa.

Via Nipashe

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527