EMMANUEL KAMARA AJAZA NA KUREJESHA FOMU UBUNGE CCM- DODOMA MJINI

Mjumbe wa Halmashauri CCM Wilaya ya Dodoma Mjini, Emmanuel Japhet Kamara (kulia) amechukua na kurejesha fomu ya kutia nia kiti cha Ubunge  ndani ya CCM Jimbo la Dodoma Mjini.

Kamara amepiga hodi katika hatua yake hiyo ya kwanza huku akisubiria maamuzi ya chama yatakayofuata.


"Nashukuru nimefanikiwa kurudisha fomu niliyoichukua na kuijaza. Namshukuru Mungu kwa kuniwezesha nguvu ya kuchukua fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea Ubunge Jimbo la Dodoma Mjini na kunipa kibali cha kuijaza na kuirudisha nikiwa salama na Malaika wake wakinizunguka", amesema

Kamara alisema sasa hatua iliyobaki ni kuwaomba Wananchi na Wanadodoma kumuombea kwa Mungu azidi kumpa uhai na afya.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527