WATU 100 WAFARIKI DUNIA KWA CORONA NDANI YA SAA 24 NCHINI UTURUKI


Karibu vifo vipya 100  vimeripotiwa ndani ya masaa 24 siku ya Jumapili nchini Uturuki, na kusababisha jumla ya vifo vinavyohusiana na ugonjwa wa Covid19 kufikia hadi 1,198 nchini, Waziri wa Afya wa Uturuki, Fahrettin Koca ametangaza.

Mbali na vifo vipya 97, kesi 4,789 mpya za maaambukizi mapya za virusi hivi, ambayo ilitokea nchini China mwezi Desemba kabla ya kusambaa hadi nchi mbalimbali duniani, zilibainika ndani ya siku moja, na kuifanya idadi ya wagonjwa kufikia 56,956 tangu kuanza kwa janaga hilo

Katika juhudi za kupambana na virusi vya Corona, Uturuki kwa mara ya kwanza ilitangaza marufuku ya kutoka nje mwishoni mwa juma lililopita


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post