POLISI ECUADOR WAKUSANYA MITAANI MAITI 800 ZA WALIOFARIKI KWA CORONA NA KUTELEKEZWA


Ecuador imesema polisi wameondoa karibu miili 800 katika wiki za karibuni kutoka katika makazi mjini Guayaquil, sehemu iliyoathiriwa kwa kiasi kikubwa na mlipuko wa virusi vya corona, baada ya ugonjwa huo kuzidi uwezo wa huduma za dharura, hospitali na kampuni za mazishi.


Wafanyakazi katika vyumba vya kuhifadhia maiti katika mji huo wa pwani wamekuwa wakishindwa kukabiliana na vifo, huku wakazi wakituma video katika mitandao ya kijamii zinazoonyesha miili iliyotelekezwa mitaani


Ecuador ambayo kisa cha kwanza cha maambukizi ya virusi vya corona kilibainika Februari 29 kwa sasa ina maambukizi 7,500 na kwamba vifo ambavyo vinahusishwa na virusi vya corona vinakadiriwa kuwa kati ya 2,500 na 3,500.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post