WAZIRI MKUU WA UINGEREZA BORIS JOHNSON AKUTWA NA VIRUSI VYA CORONA


Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson amekutwa na maambukizi ya Corona baada ya kufanyiwa vipimo, imesema ofisi yake Downing Street.



Johnson alichukuliwa vipimo vya ugonjwa huo ambao umeua zaidi ya watu elfu kumi duniani, baada ya kupata dalili kadhaa za ugonjwa wa corona.

“Nimekuwa na dalili ndogo za coronavirus, ambazo ni viwango vya juu vya joto la mwili na kikohozi ambacho hakikomi ,” Bwana Johnson amesema katika video aliyoituma kweinye ukurasa wake Twitter.

Johnson atajitenga binafsi – katika makao yake ya kikazi ya Downing Street, baada ya kupimwa na kupataikana na virusi hivyo na muhusumu wa huduma za afya nchini Uingereza katika ofisi yake al maarufu No 10.

Waziri Mkuu huyo wa Uingereza amesema kuwa ataendelea kulingoza taifa kutoka nyumbani baada ya kupatikana na Covid-19.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527