TANZANIA YAPOKEA MSAADA WA VIFAA TIBA VYA CORONA KUTOKA KWA MFANYABIASHARA WA CHINA JACK MA


Vifaa tiba vilivyotolewa na mfanyabiashara kutoka China, JackMa kwa ajili ya kupambana na virusi vya Corona nchini Tanzania vimewasili usiku wa kuamkia leo Machi 25, 2020, na ndege ya shirika la Ethiopia.


Katika taarifa yake aliyoiandika kupitia ukurasa wake wa  Twitter Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu, amemshukuru mfanyabiashara huyo pamoja na Serikali ya China kwa ujumla.

"Jana usiku sisi Tanzania tulipokea mchango wa vifaa tiba, ambavyo vitasaidia katika mapambano yetu dhidi ya COVID-19, shukrani zetu za dhati kwa mfanyabiashara JackMa na taasisi yake ya AlibabaGroup na Serikali ya Ethiopia" Ameandika Waziri Ummy.

Vifaa hivyo ni barakoa 100,000, vipimo 20,000, na mavazi ya kujilinda (protective suits) 1,000.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527