PAPA FRANCIS APIMWA CORONA


Kiongozi wa Kansa Katoliki Duniani, Papa Francis amepimwa virusi vya corona (covid-19) na kuthibitika kuwa hajaambukizwa.

Papa Francis alipimwa virusi hivyo baada ya mmoja wa wachungaji anayeishi katika katika makazi yake kugundulika kuwa na corona.

Vyombo vya habari nchini Italia viliripoti kuwa mchungaji huyo ambaye ni ofisa wa sekretarieti ya jimbo aligundulika kuwa na virusi vya corona na kuzua hofu kuwa huenda Papa Francis naye ameambukizwa.

Kwa mujibu wa tovuti rasmi ya  Vatican, mchungaji huyo alikuwa mmoja wa washiriki wa karibu wa papa na sasa amelazwa katika Hospitalini ya Roma wakati idadi ya walioambukizwa katika jimbo hilo ikifikia watano.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527