MGONJWA WA PILI APONA VIRUSI VYA UKIMWI


Kwa mara ya pili katika historia , mgonjwa aliyekuwa na virusi vya ukimwi amepona kabisa mambukizi hayo, madaktari wamesema jana. 


Watafiti wa masuala ya afya nchini Uingereza wamethibitisha kuwa yule anayetambulika kama mgonjwa wa London, ambaye aliugua kutokana na virusi vinavyosababisha ukimwi, hana tena mambukizi hayo kwa muda wa miaka miwili sasa. 

Lakini wameonya dhidi ya kuzungumzia kuhusu dawa ya kuponya ugonjwa huo. 

Katika utafiti uliochapishwa na jarida la masuala ya afya la Lancet HIV, watafiti kutoka katika chuo kikuu cha Cambridge wamesema hakuna virusi vilivyopatikana kwa mgonjwa huyo karibu miaka miwili na nusu baada ya kufanyiwa matibabu ya uhamishaji wa seli . 

Castillejo amekuwa mtu wa pili kupona virusi vya HIV.

Chanzo - DW


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527