MBOWE NA WENZAKE WAPELEKWA GEREZANI BAADA YA KUSHINDWA KULIPA FAINI


Viongozi wanane wa Chadema akiwemo mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe wamepelekwa katika gereza la Segerea kutokana na kushindwa kulipa faini ya Sh350 milioni.

Ni baada ya mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwatia hatiani katika mashtaka 12 katika ya 13 yaliyokuwa yanawakabili na kutakiwa kulipa faini hiyo lakini wameshindwa.

Uamuzi wa kuwatia hatiani umetolewa leo Jumanne Machi 10, 2020 na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama  hiyo, Thomas Simba baada ya kupitia ushahidi wa upande  wa mashtaka na ule wa utetezi.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527