KENYA YAANZA KUTEKELEZA AMRI YA WATU KUONDOKA MTAANI KUANZIA SAA MOJA USIKU KUKABILIANA NA CORONA

Amri ya kutotoka nje Nchini Kenya kuanzia saa moja usiku hadi saa kumi na moja alfajiri imeanza kutekelezwa mwendo wa saa moja huku huku wafanyakazi wa huduma muhimu pekee wakiruhusiwa kuwa nje usiku hali itakayosaidia kupunguza utangamano baina ya watu na mikusanyiko mikubwa ili kudhibiti maambukizi ya virusi vya corona.

Serikali ya Kenya imewaonya Wakenya dhidi ya kukiuka amri ya Rais ya kutotoka nje kuanzia mwendo wa saa moja jioni ambapo  maafisa wa polisi watakuwa wakifanya misako mitaani na kuwakamata wananchi watakaokuwa wakirandaranda kuanzia mwendo wa saa moja jioni. 

Mwendo wa saa kumi na mbili Wakenya wengi wameonekana wakiharakisha kuelekea nyumbani hatua iliyosababisha msongamano katika barabara kadhaa huku wale waliokuwa wakitumia magari ya umma wakionekana kusubiri katika vituo vya magari hayo licha ya muda kuyoyoma.

Hata hivyo wengine wao walikata kauli na kuanza kutembea kwa miguu wakihofia kukamatwa na maafisa wa polisi.

Mjini Mombasa na Eldoret mpango huo ulianza kwa mkosi baada ya maafisa wa polisi kukabiliaNa na wakazi saa mbili kabla ya amri hiyo kuanza kutekelezwa.

Katika mtafaruku huo waandishi wa habari pia hawakusazwa huku baadhi yao wakichapwa na polisi kwa kujaribu kurekodi katika kamera zao yaliyokuwa yakijiri.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527