SERIKALI YA CHINA YASITISHA VISA ZOTE ZA KUINGIA NCHINI CHINA NA HATI ZA UKAZI


Visa
Ubalozi wa Tanzania nchini China umeeleza kuwa kuanzia Machi 28, Serikali ya China imesitisha VISA zote za kuingia nchini China na Hati za Ukazi (residence permit), na kwamba Watanzania wenye VISA na wanafunzi wenye hati za ukazi wasitishe mipango ya kurejea China hadi itakapotangazwa.

Taarifa hiyo imechapishwa leo Machi 27, 2020, kupitia ukurasa wa twitter wa Ubalozi wa Tanzania nchini humo, hatua hii ikiwa ni kuendelea kudhibiti kuenea kwa maambukizi ya ugonjwa hatari unaosababishwa na Virusi vya Corona.

"Katika kudhibiti kuenea kwa COVID-19, kuanzia Machi 28, 2020 Serikali ya China imesitisha VISA zote za kuingia nchini China na Hati za Ukazi (residence permit), Watanzania wenye VISA na wanafunzi wenye hati za ukazi wasitishe mipango ya kurejea China hadi itakapotangazwa tena" imeeleza taarifa hiyo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527