MAREKANI YAONGOZA KATIKA IDADI YA MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA CORONA DUNIANI


Marekani imeipiku China na Italia na kuwa nchi inayoongoza duniani katika maambukizi ya virusi vya corona.


Kwa mujibu wa takwimu zilitotolewa na watafiti wa Chuo Kikuu cha John Hopkins, ni kuwa Marekani inaongoza kwa visa 83,000, ikifuatwa na China na zaidi ya 81,000 na Italia ikiwa na zaidi ya 80,000.

Kumekuwa na zaidi ya vifo 8,200 nchini Italia, ambayo ni kitovu cha mlipuko wa COVID-19 barani Ulaya, na zaidi ya 3,100 nchini China, ambako virusi hivyo vilianzia, na zaidi ya vifo 1,200 nchini Marekani. 

Wakati huo huo, viongozi wa Umoja wa Ulaya wamewapa mawaziri wa fedha wa kanda ya sarafu ya euro wiki mbili kutayarisha mpango imara wa kukabiliana na athari za kiuchumi zinazokana na janga la virusi vya corona.

 Viongozi wa nchi 27 wanachama walifanya mkutano kwa njia ya video jana na kushindwa kufikia msimamo wa pamoja kuhusu mgogoro huo.

Credit:DW


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527