Trump awafuta kazi mashahidi wawili waliokuwa katika kesi yake ya Kuvuliwa Urais

Rais Donald Trump amewafuta kazi maafisa wawili waandamizi waliotoa ushahidi dhidi yake katika kesi ya kutokuwa na imani naye iliyokuwa inamkabili.

Balozi wa Marekani kwa Muungano wa Ulaya, Gordon Sondland, amesema "Nimeambiwa kwamba rais anataka nirudi nyumbani mara moja".

Awali, Luteni kanali Alexander Vindman, mtaalamu mkuu katika masuala ya Ukraine, alisindikizwa kutoka nje ya Ikulu ya Marekani.

Inasemekana kwamba Bwana Trump amesema anataka kufanya mabadiliko baada ya bunge la Seneti kumuondolea mashtaka yaliyokuwa yanamkabili Jumatano.

Katika kura ya kihistoria iliyopigwa, Bunge la Seneti limeamua kutomuondoa rais huyo wa 45 wa Marekani madarakani kwa madai yaliyokuwa yameibuliwa dhidi yake kutokana na mahusiano yake na Ukraine.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments