WAZIRI UMMY ATOA MILIONI 2.5 KWA AJILI YA USHONAJI WA SARE 100 ZA WATOTO YATIMA SHULE YA MSINGI JIJINI TANGA


 MBUNGE wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu kushoto akimkabidhi fedha Taslimu kiasi cha Milioni 2.5 Mwenyekiti wa Kikundi cha Ushonaji cha Vijana cha Tanga Youth Tailoring Industry (Tayotai) Liliani Michael kwa ajili ya kushona sare 100 za watoto yatima wa shule za Msingi Jijini Tanga ambapo fedha hizo zimetolewa na Mbunge Ummy

 MBUNGE wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu kushoto akisisitiza jambo mara baada ya kukabidhi fedha Taslimu kiasi cha Milioni 2.5 Mwenyekiti wa Kikundi cha Ushonaji cha Vijana cha Tanga Youth Tailoring Industry (Tayotai) Liliani Michael kwa ajili ya kushona sare 100 za watoto yatima wa shule za Msingi Jijini Tanga ambapo fedha hizo zimetolewa na Mbunge Ummy

 MBUNGE wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu kushoto akisisitiza jambo mara baada ya kukabidhi fedha Taslimu kiasi cha Milioni 2.5 Mwenyekiti wa Kikundi cha Ushonaji cha Vijana cha Tanga Youth Tailoring Industry (Tayotai) Liliani Michael kwa ajili ya kushona sare 100 za watoto yatima wa shule za Msingi Jijini Tanga ambapo fedha hizo zimetolewa na Mbunge Ummy

 MBUNGE wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu kushoto akizungumza jambo mara baada ya kukabidhi fedha Taslimu kiasi cha Milioni 2.5 Mwenyekiti wa Kikundi cha Ushonaji cha Vijana cha Tanga Youth Tailoring Industry (Tayotai) Liliani Michael aliyesimama kulia kwa ajili ya kushona sare 100 za watoto yatima wa shule za Msingi Jijini Tanga ambapo fedha hizo zimetolewa na Mbunge Ummy
 MBUNGE wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu kushoto akiangalia nguo ambazo zinashonwa na kikundi hicho mara baada ya kukitembelea kulia ni Mwenyekiti wa Kikundi hicho Lilian Michael
 MBUNGE wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu katikati akiteta jambo Mwenyekiti wa Kikundi cha Ushonaji cha Vijana cha Tanga Youth Tailoring Industry (Tayotai) Liliani Michael mara baada ya kukabidhi fedha Taslimu kiasi cha Milioni 2.5 Mwenyekiti kwa ajili ya kushona sare 100 za watoto yatima wa shule za Msingi Jijini Tanga kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa na Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji
 MBUNGE wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu kulia akitazama nguo ambazo zinashonwa na  Kikundi cha Ushonaji cha Vijana cha Tanga Youth Tailoring Industry (Tayotai)  mara baada ya kukabidhi fedha Taslimu kiasi cha Milioni 2.5 Mwenyekiti  wa Kikundi hicho Lilian Michael kwa ajili ya kushona sare 100 za watoto yatima wa shule za Msingi Jijini Tanga kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa na Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji
 MBUNGE wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu kushoto akiangalia nguo zinazoshonwa na kikundi Ushonaji hicho mara baada ya kukitembela kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa na katikati mwenye shati jeuzi na mistari ni Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji
 MBUNGE wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu katikati akiteta jambo na Mwenyekiti wa Kikundi cha Ushonaji cha Vijana cha Tanga Youth Tailoring Industry (Tayotai) Liliani Michael mara baada ya kukabidhi fedha Taslimu kiasi cha Milioni 2.5 Mwenyekiti kwa ajili ya kushona sare 100 za watoto yatima wa shule za Msingi Jijini Tanga kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa na Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji


MBUNGE wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) na Waziri wa Afya MAendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto ametoa sh.milioni 2.5 kwenye kikundi cha ushonaji cha Vijana Tanga Youth Tailoring Industry (Tayotai) kwa ajili ya kushona sare 100 za wanafunzi yatima wa shule za Msingi Jijini Tanga.

Fedha hizo zimekabidhiwa na Waziri Ummy kwa Mwenyekiti wa Kikundi hicho Lilian Michael wakati alipotembelea na kujionea namna wanavyofanya shughuli zao ikiwemo changamoto ambazo wanakabiliana nazo huku akihaidi kushirikiana nao.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi fedha hizo, Mbunge Ummy alisema ametoa fedha ili kuweza kuwasaidia wanafunzi hao ambao wanakabiliwa na changamoto mbalimbali kutokana na kukosa wazazi ambao wanaweza kuwanunulia.

“Niwapongeze kwa kazi nzuri mnayoifanya hapa kwenye kikundi chenu mimi nitawaunga mkono na leo nitawakabidhi milioni 2.5 kwa ajili kuwashonea sare watoto yatima 100 kwenye Jiji la Tanga”Alisema Waziri huyo
.
Aidha pia alimtaka Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji waweke utaratibu wa watoto wanaoanza darasa la kwanza shule za msingi wapate unifomu shuleni kwa kushonewa na kikundi hiki cha vijana cha Tanga Youth Tailoring Industry (Tayotai).

“Kutokana na kwamba kikundi hiki kinafanya kazi nzuri hivyo wapeni tenda ya ajira kwani mtaji umewekwa na vifaa vipo suala lingine ni kutoa maelekezo watoto wanaonza darasa la kwanza kupata sare shuleni “Alisema

Waziri huyo alisema kwamba kikundi hicho walipewa mkopo wa milioni 100 huku akieleza kwamba sera ya maendeleo ya wanawake ambao ni sehemu ya asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halamshauri ipo chini ya wizara yake.

Alisema kwamba wasije kuwaambia Halmashauri watoe mikopo lakini hatuoni maendeleo kwenye hili huku akiwapongeza Jiji hilo kwa kutekeleza sheria ya kutenge fedha kwa ajili ya wakina mama vijana na watu wenye walemavu.

Waziri huyo alisema kwamba fedha hizo zimetoka kwa kununua vifaa na ela za uendeshaji huku akimtaka Mwenyekiti wa Kikundi hicho kuhakikisha wanafanya kazi kwa ufanisi mkubwa ili matokeo yake yaanze kuonekana.

“Kwa sasa hiyo milioni 100 mliopata kutoka Halmashauri tunachotaka irudi waweze kukopeshwa kikundi kingine sasa tumepeana muda kwa mwenendo walionao nawaombea waongezewe muda ili waweze kurejesha fedha hizo “Alisema Waziri Ummy

Awali akizungumza wakati akitoa taarifa ya mradi wa ushonaji wa Kikundi cha Vijana cha Tanga Youth Tailoring Industry (Tayotai) Mwenyekiti wa Kikundi hicho Liliani Michael alimshukuru Waziri Ummy kwa kuwasaidia kwenye kikundi hicho ambalo alisema kimeanzishwa mwezi Machi 2019 kikiwa na jumla ya wanachama 32 wakiwa ni wasichana.

Alisema kikundi hicho kinajishughulisha na ushonaji wa cherehani ambapo kinashona nguo na mitindo tofauti kwa makundi yote huku akieleza lengo la mradi huo ni kuimarisha maisha ya wanachama kiuchumi na kijamii.

“Lakini pia kutoa suluhisho la tatizo la ajira kwa vijana ikiwemo kusaidia kutatua changamoto za kijamii sambamba na kutekeleza kwa vitendo kauli mbiu ya serikali ya awamu ya tano inayo ongozwa na Rais Dkt John Magufuli kuelekea uchumi wa viwanda kufikia uchumi wa kati ifikapo 2025”Alisema

Mwenyekiti huyo alisema kwamba ili kufikia malengo yao waliwa silisha maombi kwa Halamshauri ya Jiji la Tanga ili wapatiwe mkopo kupitia asilimia 10 ya mapato yake ya ndani.

“Hivyo Halmashauri imetupatia mkopo wa milioni 100 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya ushonaji vya kisasa pamoja na mtaji wa kuanzia biashara kupitia mkopo Halmashauri ilikiwezesha kikundi chetu kwa kutununulia vifaa kama vile Cherahani za kisasa za kushonea 35, Overlock 1, Mashine ya kudarizi mashuka na vitambaa 3, kudarizi nguo 2, kufuma masweta 2,kuweka nembo 2,kushona vifungo 1,kugongesha vifungo 3 na kutupatia fedha taslimu kwa ajili ya uendeshaji “Alisema

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527