MO DWJI AIBUKA NA JIPYA BAADA YA KUTANGAZA KUJIUZULU SIMBA SC


Baada ya jana kupitia ukurasa wake wa twitter kuandika kwamba anaondoka kwenye nafasi ya kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Simba kutokana na timu hiyo kupoteza mchezo wa fainali kwa kufungwa bao 1-0 na Mtibwa Sugar, leo Mo amekuja na maamuzi mapya kwamba kilichotokea kwenye Account yake jana ilikuwa ni bahati mbaya. 


 “Kilichotokea kwenye akaunti zangu jana kilikuwa ni bahati mbaya, tuko pamoja, tunarudi kwenye ligi tukiwa na nguvu , tunajipanga kwa ajili ya ligi, nawapongeza Mtibwa kwa kuchukua kombe, mimi ni Simba damudamu, nitabaki kuwa Simba”.Ameandika Mo Dewj 



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527