MEYA MWITA AIFUTA KESI YAKE YA KUPINGA KUVULIWA UMEYA


Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeifuta kwa gharama kesi ya Meya wa jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita ya kutaka kusitisha mchakato wa kumuondoa madarakani.

Hatua hiyo inatokana na Mwita kuwasilisha maombi hayo kupitia Wakili wake Hekima Mwasipu mbele ya Hakimu Mkazi Janeth Mtega.

Wakili Mwasipu ameieleza mahakama kwamba miongoni mwa sababu zao ni kwamba anaona kesi hiyo haina maana kuwepo mahakamani kwa sababu hatua za kumng’oa madarakani zilishafanyika.

Pia muombaji (Mwita) hakupewa nafasi ya kusikilizwa mahakamani, hivyo anaomba kuliondoa shauri hilo bila gharama.

Hata hivyo, Wakili wa Serikali Rashid Mohammed amedai kuwa hawana pingamizi na maombi hayo ila wanaomba suala la gharama liwepo kwa sababu wamepoteza muda, rasilimali na uandaaji wa majibu kuhusu shauri hilo.

Katika uamuzi wake Hakimu Mtega amesema “Nakubaliana na maombi ya muombaji (Mwita) ya kuliondoa shauri hili, hivyo naliondoa kwa gharama”.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527