MFUMUKO WA BEI WA TAIFA WAONGEZEKA KWA ASILIMIA 3.8% KUTOKA ASILIMIA 3.6%

Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.

Mfumuko wa bei wa Taifa kwa mwaka ulioishia mwezi novemba 2019 umeongezeka hadi asilimia 3.8 kutoka asilimia 3.6 kwa mwaka ulioishia mwezi oktoba 2019.

Hayo yamebainishwa na  kaimu mkurugenzi sensa ya watu na takwimu za jamii ofisi ya taifa ya takwimu, Ruth Davison Minja ambapo  amesema kuwa kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma kwa mwaka ulioishia mwezi Novemba 2019 imeongezeka ikilinganishwa na kasi iliyokuwepo kwa mwaka ulioishia mwezi Oktoba 2019.

Aidha,mfumuko wa bei wa bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa mwaka ulioishia mwezi Novemba 2019 umeongezeka hadi asilimia 6.1 kutoka asilimia 5.1 kwa mwaka ulioishia mwezi oktoba 2019.

Vilevile,  Bi.Ruth amesema hali ya mfumuko wa bei kwa baadhi ya nchi za afrika mashariki Kenya na Uganda umeonekana Kuongezeka ambapo  Nchini Kenya Umeongezeka kwa asilimia  5.56 kutoka asilimia 4.95 huku Uganda ukiongezeka kwa  asilimia  3.0 kutoka asilimia 2.5.

Ofisi ya taifa ya takwimu (NBS) ni taasisi ya umma iliyoanzishwa kwa sheria ya takwimu kwa mwaka 2015 pamoja na mapitio yake ya mwaka 2018 kwa mujibu wa sheria hiyo, NBS imepewa mamlaka ya kutoa, kusimamia na kuratibu upatikanaji wa taarifa za kitakwimu nchini ikiwa ni pamoja na takwimu za mfumuko wa bei kwa ajili ya matumizi ya serikali na wadau wa takwimu.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527