MAMA MATATANI KWA KUMUUZA MTOTO WAKE


Gari la Polisi nchini Kenya

Mwanamke mmoja aliyetambulika kwa jina la Sharon Achieng (23) kutokea nchini Kenya, amekamatwa na polisi katika kituo cha Siaya kwa kosa la kutaka kumuuza mwanaye wa kiume aliye na umri miaka mitano.

Mtuhumiwa huyo alikamatwa kutokea kijiji cha Anduro, ambapo alitaka kumuuza mwanaye kwa mwanamke aliyejulikana kwa jina la Irene, kwa shilingi milioni 2 za Kenya sawa na milioni 45 pesa ya kitanzania.

Joseph Aloo ambaye ni kiongozi msaidizi wa kituo hicho cha polisi amesema, wanamshikilia mtuhumiwa huyo kwa kujaribu kumuuza mwanaye kwa mtu ambaye anafanya kazi ya ulinzi.

Pia anajitetea kwa kusema alikuwa anashindwa kumlea mtoto huyo peke yake kwa kuwa mume wake amemkimbia.

Aidha kwa upande wa Irene ambaye alipelekewa mtoto huyo ili kumnunua ameeleza kuwa, Sharon Achieng alimleta mtoto huyo huku akisema yeye ni yatima na anaishi kwa bibi yake pia hajawahi kuolewa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527