KAULI YA HUMPHREY POLEPOLE BAADA YA SUMAYE KUNG'OKA CHADEMA


Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole amemwambia Waziri Mkuu Mstaafu Frederick Sumaye kuwa alimueleza asingeweza kupata kazi ya kushauri chama chochote cha siasa kama angekuwa nje ya Chama Cha Mapinduzi.

Polepole ametoa kauli hiyo saa chache baada ya Waziri Mkuu Mstaafu Frederick Sumaye kutangaza kujiondoa ndani ya CHADEMA kwa kile alichokidai kuwa hakuna demokrasia ya kweli.


Polepole ameandika; Mzee nilikwambia, kazi ya ushauri hutaipata ukiwa nje ya CCM wenzako wanaotushauri na tunazingatia ushauri wao kwasababu tunawaheshimu, ni wana CCM na kiitikadi tuko pamoja. Sasa umebaki bila Itikadi. Ile ni mali ya Mtu ni yake, nilikwambia mwache, ona sasa unahama mara ya pili
🙆🏽‍♂️



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527