BAADA YA SUMAYE, KIGOGO MWINGINE CHADEMA ATANGAZA KUJIUZULU


Mratibu wa CHADEMA  Kanda ya Pwani, Casmir Mabina amewasilisha barua makao makuu ya chama hicho ya kujiuzulu nafasi hiyo kutokana na yaliyotokea kwenye uchaguzi wa kanda hiyo ambayo yamemfanya aliyekuwa mgombea uenyekiti, Fredreck Sumaye atangaze kukihama chama hicho.


Mabina ameeleza uamuzi wake huo leo Jumatano Desemba 4, 2019 katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.


“Haya Mambo yametokea ndani ya eneo langu la kazi na kwa maana hiyo leo Jumatano nimewasilisha barua ya kujiuzulu nafasi yangu.

"Nitabaki kuwa mwanachama mwaminifu wa chama chetu na nitakuwa tayari kutoa ushirikiano wowote utakaohitajika.” Amesema


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527