CUF KUREJESHA OFISI ZAKE ZOTE ZILIZOCHUKULIWA NA CHAMA CHA ACT WAZALENDO

Chama cha Wananchi CUF kimesema kuwa kimeazimia kurejesha ofisi zake zote zilizochukuliwa na chama cha ACT Wazalendo hususan Visiwani Zanzibar.

Kauli hiyo imetolewa jana jijini Dar es Salaama na Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini wa chama hicho, Mussa Haji Kombo, ambaye alisema kuwa ofisi hizo ni mali ya CUF hivyo ni lazima wazirejeshe.

“Kwa kuwa baraza Kuu la Uongozi la Taifa la CUF limeazimia kurejesha ofisi  zake zilizoporwa na ACT kupitia kikao chake cha hivi karibuni sisi viongozi tutazirejesha na tupo tayari kwa lolote na wala hatuna hofu na vitisho vya Maalim Seif na wafuasi wake.

Katika hatua nyingine, Kombo alimtuhumu Maalim Seif kuwa ni mbaguzi na mwenye kupandikiza chuki miongoni mwa jamii ya watanzania.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527