MIAKA MINNE YA RAIS MAGUFULI MADARAKANI

Makala Imeandaliwa na; Robert PJN Kaseko

Leo ni Kumbukumbu Muhimu sana  Kwetu Watanzania tokea Kipenzi Chetu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt J.P. Magufuli na Makamu wake Mhe. Mama Samia Suluhu Hassan waingie Madarakani Mnamo tarehe 05 Novemba, 2019. Na leo Wametimiza Miaka Minne (4) ya Utumishi wao.


Kama Taifa, tunajivunia Utumishi wao Uliotukuka na Kwa Muda Mchache Tumepata Mafanikio Makubwa sana Katika Kuitekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi.

Rais Magufuli na Serikali yake wamefanya Kazi Kubwa sana ya Kufanya Mapinduzi Makubwa Katika Sekta zote na Kuleta Maendeleo zaidi ya Matarajio ya wengi ( Beyond Expectations ). 

Baada ya Rais Magufuli Kuingia Madarakani pamoja na Serikali yake wengi walibeza na kusema tulishazoea na  hawana jipya, wapiga madili, Mfumo wa CCM na Serikali utambana hata kama alikuwa Mtendaji Mzuri Katika Nafasi ya Uwaziri, akiwa Rais hawezi kufanya lolote eti ni sawa na Mtu yuleyule

Mzee Mwenye slogan yake ya Hapa Kazi alipoanza Kupindua Meza na Kuchomoa betri ameushangaza Ulimwengu. Walisema nguvu ya soda lakini mpaka leo anatembea Katika Kasi ileile, Hadi leo Kazi Kubwa imefanyika Katika Taifa letu, Miradi Mikubwa imeendelea Kutekelezwa Nchini.

Naomba nikutajie sehemu ya Utekelezaji huo;
Ujenzi wa Mradi Mkubwa wa Kuzalisha Umeme wa Julius Nyerere ( Megawati 2115 ) Stiggler's Gorge -  Mto Rufiji ( Utagharimu zaidi ya Trilioni 6.5 hadi kukamilika kwake Ikiwa ni Kodi za Watanzania ),  Serikali imefanya kazi kubwa ya Kulihuisha na Kuliimarisha Shirika la Usafiri wa Anga ( ATCL ) Ikiwa ni Moja ya  Mikakati Muhimu wa Kuimarisha Uchumi Kupitia Sekta za Usafiri wa Anga na Utalii. 

Jumla ya Ndege Saba Mpya zimenunuliwa Kwa Mabilioni ya Pesa yatokanayo na Kodi za Watanzania; Bombardier 3, Airbus 2 na Dreamliners 2 ) 💪🏼 Ndege zote zimekodishwa Kwa Shirika letu la ATCL na Biashara inaendelea vizuri sana.

Tunajivunia Mapinduzi Makubwa yaliyofanywa na Rais Magufuli na Serikali yake Katika Sekta ya Afya ambapo Ule Mpango wa Kujenga Vituo Vya Afya Kila Kata Nchini, Hospitali za Wilaya/Halmashauri  na Rufaa Kwa maeneo yasiyo na Huduma hizo unaendelea Kutekelezwa kisawasawa. Zaidi ya Vituo Vya Afya  300  Vimejengwa na Baadhi kukarabatiwa/ Kuboreshwa. 

Hospitali za Halmashauri/ Wilaya 67 Zimejengwa nk. Mradi wa Ujenzi wa Mradi wa Barabara za Juu/ Daraja la Juu Ubungo ( Ubungo Interchange ) Mradi utakao gharimu zaidi ya Bilioni 200 Pesa za Kitanzania na Maendeleo ya Mradi ni zaidi ya 50% - Mbioni Kukamilika, Mradi wa Ujenzi wa Daraja Ziwa Afrika Mashariki ( Ziwa Victoria ) litakalo unganisha Mikoa ya Geita na Mwanza ( Busisi - Busisi ) Kilomita 3.2, Mradi huu umepangwa kugharimu Bilioni 699.9 Pesa za Kitanzania hadi Kukamilika kwake, Juzi nimepita Pale Mto wami Kazi ya Ujenzi wa Mradi wa Daraja la Mto Wami Inaendelea. 

Jumla ya Bilioni 71.4 Pesa za Kitanzania zitatumika Kukamilisha Mradi huu ambapo pia Barabara yenye urefu wa Kilomita 4.3 ya Lami itajengwa kila upande wa Daraja hili la Mto Wami kutokea hapo.( Ni kazi tuu hakuna kulemba 💪🏼).

 Tusisahau Miradi Mikubwa ya Kuimarisha Miundo mbinu wezeshi  ya Uchumi inayoendelea kutekelezwa na Serikali hii ya Awamu ya Tanu Chini ya Dkt. John Magufuli. 

Mfano Serikali kupitia TARURA na TANROADS imeendelea Kujenga Barabara za Lami zenye Ubora wa Hali ya Juu Kama ule Mradi wa Upanuzi Barabara ya Kumara - Kibaha kwa Njia Sita  ( 19.2 Kilomita ) Mradi utakaogharimu zaidi ya   Bilioni 140.44 Pesa za Kitanzania, Zile Barabara za Arusha za Mchepuo ( Arusha By-Pass 42.2 Kilomita ) na Ujenzi wa Barabara za Njia Nne Kutokea Pale Ngaramtoni hadi USA River 14.1 Kilomita na   ambazo zimekamilika na zinatoa Huduma bora kabisa haja Jijini Kwetu Arusha. Zaidi ya Bilioni 85 zimetumika Kuboresha Maisha ya Wananchi wa Arusha.

 Ebwana Tusisahau Miradi Mikubwa ya Maji inayotekelezwa na Serikali yetu tukufu Nchini Kote, Mfano mmoja miongoni mwa mingi ni huu Mradi wetu Mkubwa wa Maji  Unaotekelezwa hapa Arusha utakaogharimu Bilioni 520 Pesa za Kitanzania. 

Nimalizie kwa kutaja iliyofanyika Katika Kufanya Mapinduzi Makubwa Katika Sekta ya Nishati na Madini. Mabadiriko Makubwa ya Sharia ya Madini yamefanywa na Bunge letu Tukufu ili kuhakikisha Madini yetu yanatunufaisha Watanzania na niseme tu site tulishuhudia Sakata la Makinikia ambapo hadi mwisho Wahusika tamka Kuilipa Serikali yetu Mabilioni ya Pesa kama fidia dhidi ya Unyonyaji Mkubwa uliofanywa na Mabeberu.

Yapo mengi yaliyotekelezwa na Serikali ya Rais Magufuli toka Rais wetu ameingia Madarakani  Novemba 05, 2015. 

Kama Taifa Tumepiga hatua kubwa sana Kimaendeleo. Uchumi wetu umeendelea Kukua Kwa Kasi sana na Mambo yanaonekana Kwa Macho.

Watanzania tusidanganywe na Upotoshaji mkubwa unaofanywa na baadhi ya watu. Hawana lolote zaidi ya Kutuvuruga na Ukweli ni Kwamba Watanzania tulikuwa na Kiu kubwa ya Kuona siasa zetu zinabadirika na Kuwa siasa zinazojikita katika Kuleta Maendeleo kwa Watanzania na Kutatua Changamoto na Kero mbali mbali zinazo wakabili Watanzania, na Mungu ametujalia Kumpata Rais ambaye akiahidi anatekeleza Kwa Vitendo, anachapa Kazi tu. 

Anasimamia Vizuri sana Ukusanyaji wa Mapato na Matumizi ya Serikali. Anasimamia VIZURI sana na kwa Uaminifu Mkubwa Raslimali za Taifa letu na Kuhakikisha Zinawanufaisha Watanzania wa Sasa na Vizazi Vijavyo.

Rai yangu kwa Watanzania wenzangu; Tumshukuru Mungu kwa Kutupatia Kiongozi Mzalendo, Mchapa Kazi, Msikivu katika Kusikiliza na Kutatua Kero na Changamoto za Wananchi wake, asiyetishika wala Kuyumbishwa, Jasiri na Mwenye hofu ya Mungu. Tuendelee Kumuombea Rais wetu Afya njema, Maisha Marefu na nguvu kubwa zaidi ya Kufanya Makubwa zaidi ya Haya.

MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU MMBARIKI RAIS MAGUFULI NA WASAIDI WAKE WOTE, AMEN.

Robert PJN Kaseko
Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Arusha.
Novemba 05, 2019.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527