MTUMISHI WA AFYA AJINYONGA KWA WAYA JUU YA MTI KAHAMA

Mtumishi wa afya kituo cha afya Ushetu wilayani Kahama,Moses Amasha Mbilinyi (26) amefariki dunia kwa kunyonga kwa kutumia waya wa Extension juu ya mti nje ya nyumba aliyopanga.

Kwa Mujibu wa Kaimu Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga Adax Majaliwa tukio hilo limetokea Septemba 29,2019 majira kati ya saa tisa hadi saa 11 alfajiri katika kijiji cha Mbika kata ya Ushetu halmashauri ya Ushetu wilayani Kahama.

"Moses Amasha Mbilinyi ambaye ni nurse assistant katika kituo cha afya Ushetu amekufa baada kujinyonga kwenye mti na kuacha ujumbe wa maandishi usemao "chanda ,kama kikitokea chochote nimeacha viwanja viwili kahama anavijua malubalo, viwili nyamilangano,kimoja sijalipia laki tano hivyo ni mali ya Nancy",ameeleza Kamanda Majaliwa

Amesema chanzo cha tukio inasemekana ni msongo wa mawazo.

Na Kadama Malunde - Malunde1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527