WALICHOKISEMA CHADEMA KUHUSU BARUA YA MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA


Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimekiri kupokea barua ya Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini kuhusu Uchaguzi Mkuu wa ndani wa Chama hicho, na kusema Chama hicho hakijakiuka Sheria ya Vyama vya Siasa Nchini wala Katiba ya Chama.

CHADEMA wamesema Katiba ya Chama hicho, ibara ya 6.3.3 (a) inatoa mamlaka kwa Kamati Kusogeza mbele uchaguzi mkuu wa ndani ya Chama, na kwamba Mamlaka ya kufanya marekebisho hayo yameachwa kwa Kamati Kuu .

CHADEMA wamesema Kamati Kuu ya Chama ilikaa katika kikao chake cha tarehe 27 na 28, Julai, 2019, na kurekebisha ratiba ya uchaguzi ambapo utakamilika mwezi Disemba kwa ngazi ya Taifa na Katika hatua ya sasa, Chama kinaifanyia kazi barua hiyo ili iweze kuifikia Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ndani ya muda husika uliotajwa.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527