TANZANIA YASAINI MKATABA WA MABILIONI YA PESA KUPELEKA HUDUMA YA INTERNET BURUNDI


Kampuni ya mawasiliano ya simu ya Tanzania TTCL imesaini makubaliano na kampuni ya BBS ya Burundi kuhusu kutoa huduma za mtandao wa Internet.


Mkurugenzi mkuu wa kampuni ya TTCL Bw. Waziri Kindamba amesema, Makubaliano hayo yenye thamani ya dola za kimarekani milioni 6 yatatekelezwa nchini Burundi kwa miaka 10 ijayo. 

Amesema TTCL itatoa huduma za ngazi ya juu kwa Burundi kwa kupitia vituo vyake vya Kabanga na Manyovu, Mkoa wa Kigoma.

Bw. Kindamba amesema utoaji wa huduma za Internet utarahisisha na kuboresha biashara kati ya nchi hizo mbili.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527