LUGOLA AWAONDOA KATIKA NYADHIFA ZAO VIGOGO WATATU WA JESHI LA POLISI NKASI

Waziri wa Mambo ya Ndani Kangi Lugola amewaondoa katika nyadhifa zao vigogo watatu wa polisi wa Wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa kwa madai ya kushindwa kutimiza majukumu yao.

Walioondolewa ni mkuu wa polisi Wilaya ya Nkasi, mkuu wa upelelezi wa Wilaya hiyo na mkuu wa kituo cha polisi Namanyere.

Taarifa iliyotolewa leo Ijumaa Oktoba 4, 2019 katika ukurasa wa mtandao wa kijamii wa Twitter ya wizara hiyo inaeleza kuwa Lugola amewasimamisha viongozi hao kwa kushindwa kudhibiti wizi wa ng'ombe 278 za wananchi na kuupuza taarifa zinaporipotiwa katika vituo cha polisi.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527