WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA ATANGAZA KUONDOA VIKWAZO VINAVYOWAKABILI WAFANYABIASHARA KAGERA


Waziri wa Viwanda na Biashara,Mhe. Innocent Bashungwa(Mb)Kagera ametangaza kuondoa vikwazo vinavyowakabili wafanya biashara wadogo na wa kati mkoani Kagera.

Waziri Bashungwa ametoa kauli hiyo wakati akiwa mkoani Kagera katika uzinduzi rasmi wa mwongozo wa wiki ya Kagera uliofanyika manispaa ya Bukoba mkoani Kagera.

Waziri huyo amesema ili kuweka urahisi katika biashara kwa wenye viwanda vidogo vidogo na wa kati hasa akina mama na vijana tayari serikali imeondoa kodi 54 ili waweze kufanya kazi katika mazingira mazuri yatakayowawezesha kuchangia pato la Taifa.

Waziri Bashungwa amesema awali kumekuwepo na utitiri wa kodi kwa wafanya biashara jambo lililosababisha mikwamo katika sekta hiyo.

Amewataka wafanya biashara mkoani Kagera kufanya za uzakishaji kwa kuzalisha biashara zenye tija na zenye masoko nchi za nje kwani tayari nchi mbali mbali za nje zina uhitaji na bidhaa za Tanzania.

Amewahimiza wafanya biashara hao kutumia wiki hiyo ya uwekezaji kuwa chachu ya kuzalisha bidhaa mbali mbali na kutangaza fulsa zilizopo mkoani Kagera.

Hata hivyo ametoa pongezi kubwa kwa Rais Magufuli kwa kumteua kuwa Waziri wa viwanda na biashara huku akihaidi ushirikiano mkubwa kati yake na Mkuu wa mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco Elisha Marco ili kuitangaza Kagera kuwa sehemu yenye chachu katika uchumi endelevu kwa maslahi ya watanzani wote na wawekezaji toka nje ya nchi.
Na Lydia Lugakila - Malunde1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527