WALIOFARIKI AJALI YA MOTO WA LORI LA MAFUTA MOROGORO WAFIKIA 89


Majeruhi saba kati 32 wa ajali ya lori la mafuta ya petroli iliyoanguka na kulipuka mkoani Morogoro waliokuwa wakitibiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dar es Salaam nchini Tanzania wamefariki dunia.

Hii ina maana kuwa waliofariki kutokana na ajali hiyo iliyotokea Jumamosi iliyopita ya Agosti 10, 2019 eneo la Msamvu mkoani Morogoro hadi kufikia saa 5.30 asubuhi  ya leo Alhamisi Agosti 15,2019 ni 89.

Akitoa taarifa hiyo, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano (MNH), Aminiel Aligaesha amesema kwa sasa wamebaki majeruhi 25 kati ya 46 waliopokelewa hospitalini hapo kutoka Hospitali ya Rufaa ya Morogoro.

Amesema kati ya majeruhi hao 16 wapo katika chumba cha uangalizi maalum (ICU) huku wengine tisa wakiendelea kupatiwa matibabu katika wodi maalum iliyotengwa kwa ajili ya majeruhi hao.

“Serikali imeahidi wanaozikwa Morogoro itagharamia mazishi lakini kwa wanaotaka kwenda Mikoa mingine kama Moshi, Tanga wanajigharamia wao ila serikali itatoa sanda na sanduku tu,” amesema.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527