Picha : MARAIS 12 KATI YA 16 WAHUDHURIA MKUTANO WA SADC TANZANIA


Marais wa nchi 12 wamehudhuria mkutano wa kilele wa nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Sadc) unaofanyika jijini Dar es Salaam leo Jumamosi Agosti 17, 2019 na kesho.


Mkutano huo umeanza saa 3:49 asubuhi na kuhudhuriwa na marais na mawaziri kutoka nchi wanachama, marais wastaafu, viongozi na washiriki mbalimbali.

Marais hao ni John Magufuli (Tanzania),  Cyril Ramaphosa (Afrika Kusini), Azali Assoumani (Comoro),  Danny Faure (Shelisheli),  Joao Manuel Goncalves (Angola).

Wengine ni Edgar Lungu (Zambia), Felix Tshisekedi (DRC),  Andry Rajoelina (Madagascar), Emerson Mnangagwa (Zimbabwe), Filipe Nyusi (Msumbiji) na Dk Hage Geingob (Namibia).

Nchi  ya Eswatin imewakilishwa na waziri mkuu,  Ambrose Dlamini;  Lesotho pia imewakilishwa na waziri mkuu, Motsahai Thabane  huku Malawi ikiwakilishwa na makamu wa rais sambamba na Botswana na Mauritius zilizotuma wawakilishi.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527