RAIS MAGUFULI KUZINDUA NYUMBA ZA POLISI GEITA


Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro, amewaomba wananchi wa mkoa wa Geita pamoja na maeneo jirani na mkoa huo kujitokeza kwa wingi siku ya jumatatu kwenye tukio la uzinduzi wa nyumba za makazi ya askari, uzinduzi utakaofanyika katika eneo la magogo mkoani humo.

IGP Sirro amesema kuwa, katika tukio hilo ambalo litaongozwa na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Magufuli, ambapo atazindua zaidi ya nyumba 114 zilizokwisha kamilika huku matarajio ya mradi huo ni kuwa na nyumba takribani 400 kwa nchi nzima.

Aidha, IGP Sirro amewaomba wadau mbalimbali kuendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi katika kuhakikisha askari wanaishi kwenye mazingira mazuri jambo ambalo litachangia weledi na uwajibikaji hususan kulinda maisha ya raia na mali zao.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527