Katazo La Magogo Buchani Kuwa Changamoto Dodoma

Na. Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Wafanyabiashara wa Nyama jijini Dodoma wamesema kuwa  katazo la utumiaji magogo katika ukataji wa  nyama  Ifikapo Septemba 30,2019   katika bucha itakuwa ni changamoto kubwa kwao.

Baadhi ya  wafanyabiashara Wanyama katika soko kuu la Majengo  Mkoani  Dodoma wamesema  utumiaji wa  Magogo katika ukataji wa nyama walishaizoea  enzi na enzi  hivyo katazo  la Magogo ya kukatia  nyama buchani itakuwa changamoto kunbwa kwao.

Anna Francis na Juma Abbas ni miongoni mwa wafanyabiashara wanaojihusisha na biashara ya nyama katika soko kuu la Majengo ambapo wamesema katika utumiaji  wa Mashine za kukatia nyama patakuwepo na changamoto hususan umeme unapokatika huku changamoto zingine ni  chembechembe ya vyuma.

Changamoto nyingine ambazo wamezitaja ni  gharama ya kumudu hizo mashine  kwa urahisi wa kupatikanaji kwani mara nyingi hupatikana  nje ya nchi  hususan nchi jirani ya Kenya.

Ikumbukwe kuwa  hivi karibuni Bodi ya Nyama Tanzania ilisema kuwa ifikapo Septemba 30, 2019 itakuwa mwisho kwa wauza nyama buchani kutumia magogo na endapo mtu atabainika akitumia , hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake ambapo Ofisa Usajili kutoka katika bodi hiyo, Geofrey Sosthenes  alibainisha  kuwa magogo  yanasababisha hasara ya upotevu wa nyama, kitaalamu katika kilo 100 inapotea kilo moja, ambapo kwa mwaka muuzaji hupoteza Sh. milioni 3.8 ambayo inatosha kununua machine ya kisasa ya kukatia nyama.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments